Diamond Ndiye Msanii Tajiri zaidi Kwa Sasa Africa Mashariki

Jarida la Forbes la nchini marekani limetoa wasanii matajiri zaidi duniani ,Africa na kanda mbali mbali ambapo kwa upande wa Africa mashariki.

Diamond platinum ameongoza kwa kuwa na utajiri wa dollar million 4.5 ambazo ni zaidi ya bilioni 10 za kitanzania hasa baada ya kununua Nyumba yake ya south Africa.

Vitu vingine anavyomiliki ni Majumba ya kifahari Dar,Magari ya kifahari , Berber shop, Maduka ya nguo za mitindo ya kisasa na vingine Vingi.

Amefatiwa na Dr Jose Kamilioni wa Uganda ambaye anakadiliwa kuwa na utajiri wa dollar milioni 3.9 ... Wanafatia Akothee na Jaguar anashika nafasi ya 4

Wanachokiangalia zaidi sio pesa kwenye account Bali thamani ya vitu anavyomiliki.....

Katika jarida hilo linaonyesha diamond akiwa anafanya wastani wa show 2 kwa wiki show 8 kwa mwezi na show 100 kwa mwaka ambapo show yake ya chini anakadiriwa kulipwa wastani wa dollar elfu 20,000 na show ya juu analipwa wastani wa dollar elfu 75,000 .

Mikataba yake na makampuni kama Cocacola,Vodacom na DSTV

Jarida ilo linaonyesha pia diamond anaweza vaa vitu vyenye thamani ya dollar laki 150,000 ambazo ni zaidi ya milioni 350,000,000 za tanzania mwilini mwake kwenye shoo moja ambavyo ni Pete,cheni,viatu kofia,shati na suruali na vingine.

Kiukweli huyu mwenzetu yupo kwenye another level kabisa.

Ongera kwa diamond platinum na wapenda maendeleo wote wa nchi hii tuendelee kumsaport msanii huyu aweze kufika mbali zaidi....
Previous
Next Post »